Skip to content

Jimbo la Mashariki


Jimbo la Mashariki ni mojawapo ya Majimbo matatu ya KKKT Dayosisi ya Pare kwa sehemu kubwa Jimbo linahudumu katika maeneneo ya milimani  mwa Wilaya ya Same. Jimbo lina jumla ya Sharika 11 na limegawanyika katika kanda 2;  Kanda ya Mashariki  ina Sharika za Mtii, Ngaeni, Bombo, Mramba na Ntenga   Kanda ya Maghaibi ina Sharika za Msindo, Mbaga, Mbwakweni, Marindi,  Mhezi na Mwembe.

Huduma Zetu

Katika Jimbo la Mashariki zipo huduma nyingine kando na huduma ya msingi ya kueneza Injili, huduma zitolewazo ni”

UDIAKONIA na HUDUMA ZA KIJAMII

  • Jimbo kupitia Sharika zake limekuwa likitoa huduma kwa familia zenye mazingira hatarishi kwa kuwasaidiwa Mavazi na Chakula
  • Mfuko wa Diakonia wa Jimbo ambao unatumika kusaidia watumishi wa Jimbo  wanapopata misiba, au wagonjwa.
  • Jimbo linatoa huduma kwa washokeri/wagonjwa kwa kuwatia moyo kwa Neno la Mungu, kuwapa Sakramenti na misaada mbalimbali ya kibinadamu.

HUDUMA ZA ELIMU

  • Shule ya Awali Bombo: Ni shule inayowaandaa wanafunzi kabla ya kuandikishwa darasa la kwanza, Shule hii inaendeshwa na Usharika wa Bombo

Viongozi wa Jimbo

Mch. Enirisha Mkiramweni

Mkuu wa Jimbo

Mch. David Tendwa

Msaidizi wa M/Jimbo

Bw. Christopher Kilonzo

Katibu